Mtandao wa Wanawake Watetezi wa Haki za Binadamu kwa ufadhili wa African Women Development Fund (AWDF) umeandaa mkutano wa siku mbili wadau wa haki za binadamu wafanya maamuzi na mashirika ya utetezi wa haki za binadamu kujadili na kushauriana fursa zilizopo za uwepo wa mazingira salama ya wanawake watetezi wa haki za binadamu. Mkutano huo umekutanisha wadau kutoka serikalini na asasi za kiraia ikiwa ni pamoja na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Wizara ya Sheria na Katiba, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Tume ya Haki za Binadamu na Tume ya Kurekebisha Sheria. Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali ni kama WATED, WAHEAL, LHRC, Protection International Africa. Mkutano huu unaendelea kufanyika kuanzia Leo tarehe 22 na 23 Mei 2024 mjini Morogoro.

IMETOLEWA NA MTANDAO WA WANAWAKE WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA 22 Mei, 2024

Members

78

Members Registered

Litigation

2

Cases Intervened

Projects

5

Projects Completed

Copyright © CWHRDs-Tanzania